Monday, September 16, 2013

Mambo ya kuzingatia ilikuwakaribu na watu

Ili mambo yako yawe mazuri ni bora zaidi maelewano ya ndugu,jamaa na marafiki yawe ya kiwango kikubwa.Yafuatayo ni mambo machache ya kzingatia ili kufanikisha jambo hili
(1)Penda kuongelea maslahi ya wengi kuliko maslahi binafsi.
(2)Jitahidi kutabasamu unapoongea na mtu au watu 
(3)Jitahidi kukumbuka jina la mtu au watu unapowasiliana nao.
(4)Wakati mwingi kuwa msikilizaji na pendelea kuimiza watu wajiongelee wenyewe, itasaidia kuwajua zaidi wanachopenda au kuchukia
(5)Fanya watu wengine wajione ni muhimu na kuwapa moyo kwa kila jambo

Sunday, September 15, 2013

Mashirika yanayotoa ajira bila ubabaishaji tanzania

Ifuatayo ni orodha ya mashirika,taasisi au ngo ambazo hazina uchakachuaji katika kutoa ajira/nafasi za kazi..

Imekuwa ni kawaida mashirika kutangaza ajira eti kwa sababu ya shinikizo la serikali kufanya hivyo.Kama ni ndio basi ni kitu kibaya sana maana ni kupotezeana muda na gharama unazowezakutumia katika ufuatiliaji ya interview au usaili.Orodha ni
(1)Aluminium Africa Limited-Nyerere road hichi ni kiwanda kinahusika na uzalishaji wa mabati
(2)Mantrac Tanzania-Nyerere road hawa wanahusika na mashine za katapila
(3)Kilombero Sugar Company Limited-Morogoro ni kiwanda cha uzalishaji sukari tanzania
(4)Nafasi mbalimbali zinazosimamiwa na Utumishi
(4)TANROAD
(5)Central Electrical International-Hawa ni wanahusika na wiring katika miradi mikubwa ya nyumba/maghorofa ya mashirika binafsi au ya UMMA
(6)Radi Services-Bagamoyo road ni wataalamu wa mashine za motor,transformer na generator
(7)Tanga cement-Tanga watengenezaji wa cement
(8)Mtibwa sugar-Morogoro wanahusika na uzalishaji wa sukari
(9)Tanalec Arusha-Wasukaji wa transformer
(10)Muhimbili National Hospital
(11)Delta-Nyerere road
(12)CSI

Saturday, September 14, 2013

WATENDAJI WA SERIKALINI/MASHIRIKA YA UMMA WANABOA

Imekuwa kawaida sana katika taasisi,mashirika au serikalini watendaji wake kutozingatia matakwa ya wateja.Hii inatokea sana katika utoaji huduma serikalini ni ubabaishaji mkubwa utapigwa tarehe mpaka ukate tamaa.Alafu hawazingatii muda wa kazi wa kuingia kazini na wakiingia kazini hadithi nyingi badala ya kufanya huduma. Customer care imekuwa tatizo kwa hawa watendaji please tunahitaji huduma maana msipofanya ivyo mnarudisha maendeleo nyuma maana ukichelewa kunihudumia jua wazi, kazi zingine zinasimama kwasababu ya kukusubiri ww ambae umefanya serikali ni shamba la bibi..

AJIRA HAIJAWA NGUMU KIIVYO

Tumekuwa tukitishana sana eti haaa sasa ivi ajira hamna bora kujiajiri.Yawezekana ikawa sahihi ila si kwa fani zote.Vilele kujiajiri kunahitaji mtaji mtu hawezi kumaliza tu masomo yake nakujiajiri kirahisi labda kama ni kuuza karanga au ufundi baiskeli.Lakini kama umemaliza shahada  mtu utapenda ufanye biashara kubwa.Ni kweli kunachangamoto ya kuajiriwa ila sio kiasi inavyosemwa na wengi ila ni sera mbovu ya serikali ndio chanzo cha yote haya.Maana nchi hii inaviwanda na mashirika mengi tatizo ni uendeshaji wa mashirika hayo ambayo hayazingatii taratibu za wafanyakazi kwa lengo lakujipatia faida kubwa.

Masista du

Madada wengine wanashangaza sana wanamapozi mpaka wanaboa.Unakuta dada analeta pozi utadhani labda yeye ni special sana.Utu wetu sote ni sawa mtu asijione kama yeye ndio yeye mambo yanabadilika muda wowote.Sana madada wa dzm wamesahau duniani kila mtu anapenda maisha mazuri labda kama mtu atakuwa punguani ndio anaweza asipende vitu hivi.Mapozi yamezidi sana wakati mwingine umbo baya,sura mbaya hata mvuta hana ila maringo yamezidi.Hata kama ww ni mzuri si kila mtu labda anababaika na ww kikubwa ni kujirekebisha.

Vyombo vya habari

Waandishi wengi wa kibongo wamekuwa wakitukosesha haki ya kupata habari sahihi.Hii inatokana na uoga au itikadi zao za kutetea maslai binafsi.Inapoteza matumaini kama tabia hii itaendelea bila ufumbuzi maana itatengeneza taifa lisilokuwa na watu wenye weledi wa kuelewa mazingira yao kiuchumi,kisiasa hata kisayansi maana hawana maelezo sahihi ya habari zilizopo,zilizopita au zinazo endelea.

Monday, August 5, 2013

Mbinu za kuishi na watu mbalimbali katika jamii

Kila mtu anatabia na mtazamo wake  katika maisha.Lakini ili kuenenda na tabia na mtazamo wa watu tofautitofauti.Zifuatazo ni mbinu mathubuti zikizingatiwa basi utaishi na jamii yoyote ile kwa amani.
  • Kwanza soma tabia,utamaduni na kanuni za jamii husika.
  • Msome kila mtu na tabia yake.Kwa mfano watu wengine wanapenda kusifiwa tu na wengine kila kitu yeye anajua wala hataki kupingwa.
  • Jitahidi ufanye kila kitu kwa ufanisi wa hali ya juu.uwemstaarabu mfano usikae kwenye meza wakati kiti kipo.Kifupi usifanye kitu ambacho utaonekana wa ajabu na wenzako wakakupunguzia heshima.
  • Haina aja ya kunata sana japopokuwa unamafanikio kupita wengine.
  • Kuwa mkweli na muwazi kama jambo hilo halina mslahi kwako.Sio unashabikia jambo etikisa fulani kasema.
  • Jaribu kushiki na jamii kwa jambo unalolijua au kujifunza jambo jipya ilimladi mshiriane.Hii itasaidia kuwa pamoja.Hii itakuweka karibu na jamii.
  • Usihusishe na jambo usilolipenda maana litaleta tofauti mwisho mtashindwa kuelewana.

Saturday, August 3, 2013

kamari zisizo rasmi

Hivi hizi kamari zinazochezwa nchini mbona ni wizi wa waziwazi au sheria inawalinda.Ila kama ningepata nafasi ningezuia kamari  kama karata tatu nani kaona au wanao tumia makanda  na wale wanaotumia kadi kutuibia watanzania.Ushauri wa bure kabisa tuache kupenda doze tufanye kazi japo na ajira nazo ni adimu. 

Tuesday, July 30, 2013

Sheria ya usalama barabarani

kama ni sheria bora duniani ni usalama barabarani.Sheria hii ya usalama barabarani ikifuatwa itasaidia sana.Lakini nchi yetu ubabaishaji mtupu kwa mfano gari la abiria tsh 400/= ila kwa sababu tu usafiri ni tabu mtalipa buku.Sawa kwa wakati huu usafiri ni mgumu utakuta watu wenye magari binafsi sio ya abiria wanakupiga kutoka 600 mpaka 2000 utafanyaje na sisi ndo wenye shida tunalipa ila sheria haijafanya kazi yake.Sio siri inaumiza sana maisha yenyewe bongo yako wapi wenye nacho watazidi kuwa nacho tu sisi wengine tutaendelea kusanda.

Sunday, July 28, 2013

Si sahihi

Mtazamo huu si sawa eti ukiongea ukweli utachukiwa.Hii aileti maana kwasababu tukikubaliana hivyo basi inamaana watu wanapenda kudanganywa.Msemo huu unatumika pale tu kunapo kuwa na maslahi ya watu alafu useme kweli hapo watu hao lazime wakuchue na siyo wanakuchukia kwa kusema ukweli bali  kwasababu utawahatarishia maslahi yao.Huu ndo ukweli wenyewe utaupata hapahapa tu.

Mtazamo tu

Nchi yetu sasa si nchi ile ya mwaka 47.Kwasasa Viongozi wanatakiwa wakipewa wizara basi ilingane na taaluma yake hii itasaidia utendaji bora.Huu si wakati wa ujanja ujanja hata kama unafanyika ila mwisho wake upo tu.Unapopewa dhamana na wananchi basi wajibika mbona rahisi tu.Fanya vizuri nawe ukumbukwe kama Nyerere hata kama upendi ivyo basi fanya kwasababu Mungu anaona ambavyo binadamu hawezi ona.

Freemason

Watu wengi wanaongea kuhusu freemason ila wengi hatujui ni nini?.Wapo wanasema freemason ni dini.Yawezekana ikawa ni dini ila kwa nilivyo chunguza Freemason kwa kiswahili maana yake ni Mjenzi huru.Maana yake kuna uhuru wa kuanzisha unachokitaka yaani kujenga.Jumuiya hii ni yasiri ndo maana kwa nchi za afrika haijulikani sana kama nchi za ulimwengu wa kwanza.Kiukweli jumuiya hii ni hatari sana kwa mwanadamu maana malengo yake si mazuri kwa mwanadamu.Huu ni ujanja wa shetani wa kumpa uwezo mwanadamu ili amdanganye ili waende pamoja motoni(ziwa la moto).Muovu huyu akaacha kiti chake na kumpa mwanadamu kiti hicho ili kufanya lolote amdanganye binadamu huyu.Freemason hawa wanaamini kuwa kuna nguvu ipo tu kiasili(supreme being) huyu ndo shetani kapotosha badala ya kuamini Mungu anapotosha kwamba yeye ndo ananguvu loooh Eeee Mungu utusaidie maana duniani tunayodhiki.

Saturday, July 27, 2013

Je unataaluma hiyo?

Ni bora kukaa kimya kama hujui jambo fulani sio kulopoka mwisho wasiku utaonekana huna maana.Wakatimwingine unakuta mtu mishipa imemtoka kuongea kitu hata akijui au amesikia tena kwa mtu asiye makini alafu naye anachukua pumba hizo na kubwabwaja ovyo.Ni heri tuongelee kitu tunacho fahamu au tulicho kiona.

Vyombo vya habari na mitandao isiwe sehemu ya kuonyeshana ubabe

Vyombo vya habari au mitandao ya kijamii vitumike katika kuiendeleza jamii si vinginevyo.Watu wanatumia vibaya vyombo hivi kudhalilishana na kukebehiana.Badala ya kuombana msamaha inapo bidi lakini mnatupiana maneno sijui mnaona sifa afu mtangazaji sijui anajisikiaje au ndo kushuka kwa maadili.Sio kila mtu anafurahi kujibizana kwenu.Ebu tubadilike 

Mpaka lini tutakuwa kichwa cha mwendawazimu

Kila kitu sisi tunasuasua sio michezo,siasa,elimu wala sanaa.Tatizo kubwa ni kujuana na kuacha majembe ambayo yangesonga mbele katika nyanja za kimataifa.Utakuta mtu akianzisha kitu kizuri anasongwasongwa mpaka anakata tamaa.Hata tuzo tunapeana kwa kujuana na kusababisha kutosonga mbele.


Mungu ibariki nchi yetu.

Nani mtetezi wa wanyonge

Looh inauma napoona wanyonge tunaonewa.Kuna mambo mengi tunashindwa kupata kulingana na kipato chetu.Nguvu ya uma imekuwa hadithi katika nchi zetu.Ila kinachotuponza ni uelewa mdogo miongoni mwetu.Kuna kero nyingi sana kitaa ambazo zinashindwa kutekelezwa na viongozi wetu cha ajabu bado tunaendelea kuwachagua.Kama mtu ameshindwa kutekeleza ahadi zake bila sababu za msingi apigwe chini.

Hasira

Naamini wanadamu wote tuna hasira.Ivi kuna mtu akifinywa anaweza akawa anacheka? badala ya kugugumia maumivu.Kama sio basi ndo tulivyo umbwa .Ila utakuta baadhi ya watu wanajiona hawana hasira ki ukweli tumepishana kiwango katika kuidhibiti hiyo hasira.

Thursday, July 25, 2013

MAFANIKIO

Ili kupata mafanikio ni lazima kuzingatia  kujitambua.Watu wengi wanashindwa kufikia mafanikio kwa sababu hawajui haki na wajibu wao wa msingi.Kwa hiyo ni lazima tufahamu sisi ni nani tunahaki gani katika jambo tunalolifanya kama ni mwanafunzi,mwalimu,mfanyakazi,mjasiriamali au mfanyabiashara.Ndio mambo yakuzingatia hayo sio unasitata au kuogopa kwenye haki yako.Vilevile chochote unachofanya fanya kwa moyo wote kwa asilimia mia moja mpaka wote wakubali kuwa umefanya yako..

Monday, July 15, 2013

UVAAJI HUU HATARI

Uhuru unapozidi unapelekea majanga mabaya binafsi au kwa jamii..Pitapita za kitaa zimefanya nikutanane na madada zetu mavazi wanayo vaa aibu..Unakuta dada wa ukweli ila mavazi anayo vaa ki ukweli kwa wenye maadili mema tunaona ni kujiabisha bila kujua maskini anaona katokelezea..Nani kasema ukivaa mini sketi,taiti au kuacha maungo yako ndo ujanja..Haahaa ila hawajui kwamba kizuri chajiuza na kibaya cha jitembeza..Hamna shaka jitembezeni tu ila sijui kama mtu makini kama atapenda kuoa dada wa aina hii..

Sunday, July 14, 2013

TUFUATE UTARATIBU..

Wakati mwingine nakereka sana.. Utakuta mtu kwenye mtandao wa kijamii  eti anaandika inrelationship ina maana gani  sasa tena anakuacha njia panda bora kidogo aandike inrelatioship with somebody kiasi fulani ina mantiki.Ila bora zaidi kuandika Engaged au married.

HAPO TUTAENDA SAWA..

HIVI DUNIANI HAPA TUPO KWA KUSUDI GANI??

Kila nikijiuliza kusudi la kuepo duniani napata kigugumizi .Je tumekuja kujitesa au kupingana na maumbile halisi ya kibinadamu..Ndio kwa sababu vitu vizuri vingi ni haramu au wanasema anasa.Kwa mifanano Moja ni pombe hii inapendwa na baadhi ya jamii na ni sehemu ya kiburudisho kwao;Pili ni Wanawake/Wanaume hawa wanapingwa sana ila unatakiwa kuwa naye mmoja hasa baada ya ndoa na Tatu Chakula unakuta watu wanajinyima kula eti wamefunga..

Lakini baadhi ya ivyo vina leta maana Mfano POMBE kiukweli ukizidisha pombe lazima utafanya mambo ya ajabu nakukusababishia Majuto; na Pili Wanawake/Wanaume kimsingi tukiwa waaminifu kwa kuwa na mke/mme mmoja tutaishi kwa amani na kujiamini ila ukienda tofauiti tuu inakula kwako mara eeh kaswende ,gonorhea mbaya zaidi UKIMWI.Ila hata kula kwaweza sababisha madhara mfano baadhi ya vyakula watu wana aleji navyo.Ndo maana katika uzima wa milele hakuna kula wala kunywa.

HAAAA KILA KITU DUNIANI KINAMAKUSUDI YAKE.

BINADAMU TUSHIRIKIANE.

Wakati mwingine sisi binadamu ni waajabu sana.Badala yakufikilia maisha haya tutafanyaje yawe nafuu kwa kila mtu lakini unakuta mtu anapindisha tu eti kwa kulinda itikadi zake.Dunia mapito jombaa tushirikiane kama mchwa tufike lengo..Maana utanicheka mimi leo kesho yanaweza mkuta ndugu,rafiki au kizazi chako mwenyewee..

VIJANA MUWE MACHO....

Hii ni kwa  vijana;

Kumbukeni kuwa wakati wa ujana ni wakati muhimu sana katika maisha ya  binadamu na ujana ukipita haurudi tena kamwe. Wakati wa ujana ndiyo wakati ufaao kwa ajili kujikusanyia elimu,mafunzo na taaluma mbalimbali zilizojazana chini ya jua letu.Vijana mnapaswa kutumia nafasi na nguvu zote kwa ajili ya kutimiza mambo yaliyotajwa hapo juu na kamwe msidanganyike na tamasha la ulimwengu ambalo linapita mithili ya tamithiliya.

Kila siku inayoitwa siku mpya machoni pa binadamu  ni siku mpya kwa maendeleo ya sayansi na  teknolojia yake  ambayo waathirika wake  wakubwa ni vijana kutokana na uwezo wenu wa kupokea na kuhifadhi maarifa mapya kwa haraka na kwa ufanisi mkubwa.

Wosia wangu kwenu  ni kuendelea kutumia nafasi hiyo kwa manufaa yenu; familia zenu  na maisha yenu ya kila siku. Jiandae  katika kutambua hatari zinazowakabili maishani.


Enyi vijana wa kike na kiume  tumieni mitandao kijamii kwa ajili ya kujipatia manufaa za kielimu, biashara na uchumi kwa ujumla wake na  si uwanja wa kuchokoza hisia za kimapenzi  ili kujiepusha na ngono za ujanani zinazoambatana na maambukizi ya magonjwa ya zinaa chini ya hitimisho la kifo cha mapema.






WAHENGA WALISEMA

Kuishi kwingi kuona mengi... Kila siku binadamu maarifa yana ongezeka..So tueshimiane sana sio unamuona mwenzako unamchukulia hopeless hasa mtu haumjui..